Linah: NAMPENDA MWANAUME MWENYE SIFA KAMA ZA DARASA

humph the GREAT
 darasaglobaltvonline2  
Sharif Thabiti Ramadhani ‘Darasa’
Stori: Humphrey \, blogger
DAR ES SALAAM: Mkali wa Hip Hop Bongo, Sharif Thabiti Ramadhani ‘Darasa’ amefunguka kuwa anaheshimu maneno ya msanii mwenzake, Estalina Sanga ‘Linah’ kuwa anamkubali na kutamani kuwa na mwanaume mwenye sifa kama zake lakini yeye ana mpenzi wake wa muda mrefu.
linah 
Estalina Sanga ‘Linah’
Akizungumza na Wikienda alipotembelea Global TV Online wikiendi iliyopita, Darasa alisema kuwa Linah ametumia ujasiri kutoa hisia zake na amefurahi kusikia anamkubali ingawa yeye ana mpenzi wake wa muda mrefu na wanaaminiana.

“Namshukuru kwa kunikubali, kiukweli namheshimu na nimefurahi,” alisema Darasa.
Darasa alifunguka hayo baada ya hivi karibuni Linah kueleza hisia zake kwenye mitandao ya kijamii kuwa anatamani awe na mwanaume mwenye sifa alizonazo Darasa.

Post a Comment

Please Select Embedded Mode To Show The Comment System.*

Previous Post Next Post