SERIKALI YATOA TAMKO::WAGANGA WA JADI WOTE WANAJITANGAZA KWAMBA WANATIBU MAGONJWA SUGU KAMA UKIMWI,KISUKARI KUKAMATWA



























Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii imeagiza vyombo vya dola, kukamata waganga wa jadi, wanaojitangaza kutibu magonjwa ya Ukimwi, kisukari na 
shinikizo la damu.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,
Dk Seif Rashid alipokuwa akiwasilisha bungeni hotuba ya bajeti ya

 Wizara yake 
kwa
 mwaka wa fedha 2014/15.
Aliwasihi wataalamu wa tiba asili na tiba mbadala, kuacha mara
 moja,
 kujitangaza kuwa 
na uwezo wa kutoa tiba dhidi ya ugonjwa wowote ule ambao 
uwezo huo haujathibitishwa 
kitaalamu.
“Hilo ni kosa kwa mujibu wa sheria iliyoanzisha tiba asili na tiba 

mbadala,” 
alisema.

Waziri huyo alisema yapo matangazo yanayohusu kuwa na uwezo wa 

kutibu Ukimwi,
 kisukari 
na shinikizo la damu. “Kwa mujibu wa Sheria ya Tiba asili na Tiba mbadala, matangazo 
hayo 
yaondolewe mara moja,” alisema.
Alieleza kuwa wizara itatoa mwongozo na taratibu zinazopaswa kufuatwa ili dawa husika 

zithibitishwe kitaalamu.
“Napenda kuchukua fursa hii kuagiza vyombo husika vya serikali, vifuatilie kwa karibu na 

kuchukua hatua kwa mujibu wa sheriakwa wale watakaokwenda kinyume na sheria,”
 alisema.
Waziri huyo pia alizungumzia suala la tiba za kibingwa, ili
kupunguza idadi ya wagonjwa wanaokwenda nje ya nchi kwa uchunguzi na 

matibabu.
Alisema Wizara inaendelea kuanzisha huduma za tiba za kibingwa katika hospitali za Kanda, 

hospitali Maalum na Hospitali ya Taifa Muhimbili ili kupunguzwa wagonjwa hao wa kwenda 
nje ya nchi.
Alisema huduma za upasuaji mkubwa wa moyo, zimeendelea kutolewa ambapo hadi 

sasa wagonjwa 671 walipata huduma hiyo kwa mafanikio katika hospitali za Muhimbili, 
Bungando na KCMC.
Aidha, wagonjwa 211 walifanyiwa upasuaji maalum katika 

Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI), ambapo 29 walifanyiwa upasuaji wa ubongo, 
107 upasuaji wa uti wa mgongo, 
56 waliwekewa viungo bandia vya nyonga na 19 viungo bandia vya goti.
Dk Rashid alisema katika mwaka 2014/15 Taasisi ya Mifupa Muhimbili inatarajia

 kuwahudumia wagonjwa wapatao 6,900.
Aidha, itafanya upasuaji wa kuweka viungo bandia vya nyonga kwa 

wagonjwa 400, 
kuweka viungo bandia vya goti kwa wagonjwa 150, upasuaji wa ubongo kwa
 wagonjwa 240, 
upasuaji wa uti wa mgongo na mishipa ya fahamu kwa wagonjwa 400 na upasuaji wa 
watoto 
wenye vichwa vikubwa 600.
Bajeti aliyoomba ili kuiwezesha Wizara yake kutekelezwa kazi zilizopangwa katika 

mwaka 2014/15, Waziri huyo aliomba Bunge kuidhinisha makadirio ya matumizi ya 
wizara hiyo pamoja na taasisi zake yenye Sh bilioni 622.95, ambapo kati ya hizo 
Sh bilioni 317.22 ni kwa ajili ya matumizi ya kwaida na Sh bilioni 305.72 ni 
kwa ajili
 ya
 utekelezaji wa miradi ya maendeleo

Post a Comment

Please Select Embedded Mode To Show The Comment System.*

Previous Post Next Post