Nuh Mziwanda avunja ukimya, afuta tattoo ya Shishi

humph the GREAT
Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nuh Mziwanda katika pozi

Mwanamuziki nchini Tanzania, Nuh Mziwanda, ameamua kuvunja ukimya na kufuta tattoo yenye jina la aliyekuwa mpenzi wake Zuwena Mohamed ‘Shilole’, kabla ya kupata mbadala wake.
Awali baada ya kutengana Nuh, alidai kuwa tattoo ya Shishi, haimuumizi kichwa kwa kuwa aliichora kwa mapenzi yote na sio kwa kuigiza hivyo kutengana kwao sio sababu ya kufuta tattoo hiyo.
Nuh, ameshindwa kuonesha uvumilivu kuiona tattoo hiyo na kudai kuwa baada ya kuachana na mrembo huyo amekuja kujua kuwa Shishi, hakuwa mbadala wake sahihi kwani amekuwa akimfanyia vituko mbalimbali.
Amedai kuwa mrembo huyo amekuwa akitumia mtandao wa kijamii kumtukana pia kupitia mahojiano mbalimbali jambo ambalo amekuja kujua hakuwa mtu mzuri wake
Sambamba na hilo Nuh, mbali na kuchora tatoo mpya juu ya ile ya Shishi Baby, ameongeza tatoo nyingine kadhaa mwilini kwake ikiwepo usoni.
Wawili hao wameachana siku za hivi karibuni huku kila mmoja akificha chanzo cha penzi lao kuota mizizi na hivyo kufikia hatua ya kila mtu kufuta tattoo ya jina la mpenzi wake.


 


Previous Post Next Post