humph the GREAT
nuhu mziwnda akiwa na shilole
Msanii huyo alipoulizwa kuhusu mahusiano yake kati ya yeye na shilole alikuwa hana mengi ya kuongea zaidi ya kusisitizia ni kwanini hapendi skendo kwani skendo nyingi chanzo cha kusambaa kwazo ni kuhojiwa hivyo hataki tena kuhojiwa kuhusiana ni nini hatima ya mahusiano yake kati yake na shilole
M SANII wa Bongo Fleva
anayetamba kwa sasa na Wimbo wa Jike Shupa, Naftari Mlawa ‘Nuh Mziwanda’
amesema kuwa kwa sasa amechoka kutegemea skendo za kijinga kumng’arisha
badala yake atajitahidi kuboresha kazi zake akiamini hiyo ndiyo njia
pekee ya mafanikio.
Nuh aliyasema hayo alipokuwa akipiga
stori na gazeti hili ambapo alisema kama ni skendo amefanya sana lakini
matokeo yake anaona maendeleo yake kimuziki yanajongea kwa mwendo wa
kobe suala ambalo ‘sometimez’ linamkatisha tamaa.
“Sasa nataka nikomae tu kwenye kazi
yangu ya muziki, kiki za kijinga hazina faida, watu wanataka muziki
mzuri tu na ndicho nitakachofanya ili niwakune mashabiki wangu,” alisema
Nuh.
nuhu mziwnda akiwa na shilole
Msanii huyo alipoulizwa kuhusu mahusiano yake kati ya yeye na shilole alikuwa hana mengi ya kuongea zaidi ya kusisitizia ni kwanini hapendi skendo kwani skendo nyingi chanzo cha kusambaa kwazo ni kuhojiwa hivyo hataki tena kuhojiwa kuhusiana ni nini hatima ya mahusiano yake kati yake na shilole
Tags
Burudani