Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Ticker

6/recent/ticker-posts

Baadhi ya wabunge wathibitisha ugonjwa wa mhe. mbowe

humph the GREAT


MBUNGE wa Kilombero (Chadema), Peter Lijualikali amelieleza Bunge, Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe hakushambuliwa na watu wasiojulikana bali alidondoka katika ngazi akiwa amelewa. Amewatuhumu Chadema, kucheza michezo ovu dhidi ya Serikali.

“Jana limetokea jambo, Msigwa Peter anasema jana mpaka saa 3 walikuwa kwa Mwenyekiti na baadaye akatoka, walienda kunywa Pombe, walienda kulewa na hata tukio sisi tunajua Mh. Freeman Mbowe kapanda ngazi kateleza kavunjika, huu ni ukweli kabisa.

“Hivi inawezekanaje KUB atembee usiku wa manane bila ulinzi na ni chama chenye umakini, mnasema hizi ndiyo akili mbadala, tungekaa kimya ila kwa sababu wameisingizia Serikali eti wameshambuliwa Kisiasa, mtu anataka akuzuie uchaguzi akuvunje leo.

“Watanzania naomba mfahamu hii michezo inafanyika na ukitaka kujua kama ni usanii, kwa nini kaenda Ntyuka na siyo General Hospital, kwa sababu alijua akiwa Serikalini pale watasema alikuwa amelewa, ninavyoongea saa hivi Ntyuka pale hayupo keshakimbia tayari,” amesema Lijualikali.

Post a Comment

0 Comments