Kundi la Bongo Movie Unit ambalo linaundwa na baadhi ya wasanii wa filamu Swahiliwood leo limetoa msaada wa vitu mbalimbali katika hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es salaam. Kundi hilo lilitoa msaada huo kwa ushirikiano wa kampuni ya Mabibo Beer(wauzaji wa vinywaji vya Windhoek na Climax) ambayo inadhamini maadhimisho ya miaka mitatu tangu kuundwa kwa kundi hilo ambalo kwasasa mwenyekiti wake ni Steve Nyerere.
Tags
Bongo movie