Dawati Concert… AY, FA, Ben Pol kukiwasha Dar Live leo

humph the GREAT
8&9 amani copy                                                   
ayy
   Ambwene Yessaya ‘AY’
WAKALI kibao wanaokimbiza kunako Muziki wa Bongo Fleva wakiongozwa na AY, MwanaFA, Ben Pol, Barnaba wanatarajiwa kuangusha bonge la shoo lililopewa jina la Dawati Concert leo ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live uliopo Mbagala- Zakhem jijini Dar.

mwana_FA-360x542                                                          Mwana FA
Akizungumza na Risasi BMM mratibu wa shoo hiyo iliyopewa jina maalum la Dawati Concert, Arthur Samuel alisema kuwa, shoo hiyo imekuja ikiwa suala la uchangiaji wa madawati kwa shule mbalimbali nchini likishika hatamu karibu kila sekta na lengo lao ni kukusanya fedha za kuchangia madawati ili wanafunzi wapate mazingira bora ya kusomea.

barnaba1                                                             Barnaba
“Kama mtakumbuka hili suala la kuchangia madawati ni moja ya kauli mbiu za Rais Dk. John Pombe Magufuli. Niwaombe mashabiki wa burudani hasa muziki huu wa Bongo Fleva wajitokeze kwa wingi kujumuika nasi,” alisema Arthur.

Linex-                                                          Linex
Arthur aliongeza kuwa fedha zitakazokusanywa katika ‘event’ hiyo itakayoanza saa 12 jioni, zote zitaingizwa katika mradi huo na kwamba wasanii maarufu walioguswa na suala zima la elimu wanajitokeza kuperform bure na kukonga nyoyo za mashsabiki

msami                                                             Msami
“Utakapohudhuria shoo hii ya kiingilio cha Sh. 5,000 tu, utakuwa umeingia moja kwa moja katika kuchangia fedha za madawati kwa watoto wetu, wadogo, ndugu na jamaa zetu mbalimbali ili wapate elimu nzuri.

Mc-Pilipili                                                         MC Pilipili
“Wasanii watakuwepo kibao kama, Ambwene Yesaya ‘AY’, Mwana FA, Barnaba, Linex, Msami a.k.a Mabawa, Glorious Worship Team, Galatone a.k.a Mzee wa Samaki, mchekeshaji maarufu wa majukwaani, MC Pilipili, Ben Pol na wengine wengi na wote hawa watafanya shoo ya kiingilio cha shilingi 5,000 tu ambapo hawatachukua chochote katika fedha itakayopatikana, kwa maana kwamba yote itakusanywa kununulia madawati na kuyapeleka sehemu husika

zbenpol                                                                                          Ben Pol
“Haya madawati hayatalenga shule za Dar tu, tutaangalia maeneo mbalimbali Tanzania nzima, kuwa wapi panapohitajika huduma hii kwa haraka zaidi ndipo tutakapopafikia mapema zaidi. Kwa kupitia shoo hii tunaamini watu wa burudani wamepata sehemu ya kuwasilisha michango yao katika elimu,” anamaliza Arthur.

Post a Comment

Please Select Embedded Mode To Show The Comment System.*

Previous Post Next Post