humph the GREAT
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Abubakar Chande maarufu kama 'Dogo
Janja' ambaye pia ni mume wa msanii wa filamu nchini Irene Uwoya
amefunguka na kudai mwanamke hata awe na pesa kiasi gani hawezi kupenda
mwanaume asiyekuwa na muelekeo wa maisha.
Dogo Janja ametoa kauli hiyo siku za hivi karibuni wakati alipokuwa
anazungumza kwenye kipindi cha DADAZ kinachorushwa na tinga namba moja
kwa vijana EATV kila siku ya Jumatano kuanzia saa 5:00 asubuhi hadi 6:00
mchana baada ya kuulizwa kuwa ni kweli wanaume wengi wanaogopa kuwa na
wanawake waliowazi kipato.
"Mwanamke hata awe na hela vipi hawezi kuwa na mwanaume asiye na
muelekeo kwani mara nyingi huwa wanapenda akiwa na rafiki zao basi awe
'proud' na mtu aliyenae", amesema Dogo Janja.
Pamoja na hayo, Dogo Janja ameendelea kwa kusisitizia baadhi ya mambo
kuwa "wanaume wanapaswa wawe 'real' yani wawazi katika mahusiano yao na
sio kuishi katika maisha ya kujidanganya, kwani inaweza kuwapelekea
kupata hasara na kuumbuka".
0 Comments