Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Ticker

6/recent/ticker-posts

hivi ni jinsi ya kuhifadhi homoni mwilini

humph the GREAT
humph the GREAT

Wanawake ambao wamewahi kupotea uja uzito au waliovuja damu katika miezi ya awali ya uja uzito wanaweza kuimarisha nafasi yao kujifungua salama iwapo watapewa homoni ya progesterone, utafiti unaonyesha. 

Watafiti nchini Uingereza wamefanya majaribio kwa wanawake 4000 wenye mimba.
Samantha Allen, mwenye umri wa miaka 31, alianza kuvuja damu alipompoteza mwanawe wa kwanza na alifanya hivyo tena alipokuwa mja mzito kwa mara ya pili.
Badaa ya kupewa homoni hiyo kwa wiki naneo, almzaa mwanawe wa kiume Noah.

Progesterone ni homoni muhimu wakati wa uja uzito - inayotumika kuimarisha uzio wa kizazi ambako sehemu ambako kijusi kinajiambatanisha na kusaidia mfumo wa kinga mwilini.
Samantha alipewa tembe za homoni ya progesterone kwa majaribio , ambazo alizitumia mara mbili kwa siku mapaka alipotimiza wiki 16 za uja uzito.

Alisema aliacha kuvuja damu wiki moja tangu aaanze kutumia tembe hizo na aliendelea vizuri na uja uzito wake.

"Natumai hawatoteseka tena, inakuathiri sana," amesema.
Mwanamke mmoja kati ya watano hupoteza mimba, na mara nyingi uvujaji damu unahusishwa na kuongezeka hatari ya mwanamke kupoteza uja uzito.
wakati homni hiyotayari imetumika katika mfumo wa kupachika mimba, IVF, Samantha anasema hakuwa na shida yoyote kushiriki katika utafiti huo.
"Ninafurahi, sikuhisi hatari yoyote kwasbabu yalikuwa hayakuwa majaribio ya kiwango cha awali."
Utafiti huo wa chuo kikuu cha Birmingham uliochapishwa katika jarida la afya la New England, umewahusisha kundi la wanawake 200 waja wazito waliopewa homoni ya progesterone, huku kundi jingine la wanaawake kama hao wakipewa tembe bandia.
Wote walikuwa wanavuja damu katika miezi ya kwanza ya uja uzito.

Licha ya kamba utafiti huo umeonyesha sio wanawake wote wanaovuja damu katika siku za kwanza wanaweza kusaidiwa kwa kutumia homoni hiyo, manufaa hayoni makubwa miongoni mwa wanawake walio na historia ya kupoteza uja uzito. (Watoto watatu au zaidi)
Miongoni mwa wanawake hao, kulikuwa na ongezeko la 15% la wanawake waliojifungua - huku 98 kati ya 137 wakifanikiwa kujifungua ikilinganihswa na 85 kati ya 148 waliopewa tembe hizo bandia.
Arri Coomarasamy, daktari wa afya ya uzazi katika hospitali ya akina mama na watoto Birmingham amesema matibabu hayo huenda yakasaidia kuokoa maisha ya maelfu ya watoto.
Ameendelea kueleza kwamba matibabu hayo hatahivyo hayatofanya kazi kwa wanawake wanaopteza uja uzito, kwasababu kuna sababu nyingi na ngumu kuhusu kwanini wanawake hupoteza uja uzito.
Ni wanawake walio na tatizo la upungufu wa homoni ndio wanaoweza kufaidika.


Serikali ya Tanzania haitaongeza muda wa likizo ya uzazi , limeripoti gazeti la binafsi la The Citizen nchini humo.
Naibu waziri wa afya Faustin Ndugulile ameliambia bunge kuwa wanawake wanaojifungua mtoto mmoja wataendela kupewa 84 za likizo ya uzazi huku wanaojifungua watoto mapacha wakipata likizo ya siku 100, limeeleza gazeti hilo.
Dr Ndugulile alikuwa akijibu swali kutoka kwa Mbunge wa chama kikuu cha upinzani Chadema Grace Tendega Jumanne ambaye aliiuliza serikali iwapo ina mipango ya kuongeza siku za likizo kwa akinamamawanaojifungua watoto njiti, linasema gazeti hilo linalochapishwa kiola siku.
Naibu waziri alisema kuwa wanawake wanaonyonyesha watapewa saa mbili kwa siku na kwamba serikali itaendelea kutekeleza sera yake ya afya ya mwaka 2007 juu ya vipengele vya huduma bure za afya kwa makundi maalumu, wakiwemo wanawake wajawazito , limesema The Citizens.

Je gharama ya uzazi katika baadhi ya mataifa Afrika mashariki ikoje?

Kwa mujibu wa shirika la afya duniani WHO, takriban wanawake 830 hufariki kutokana na sababu zinazoweza kuepukika zinazohusiana na uja uzito na kujifungua ikiwemo gharama za kupokea hudumu za afya.
99% ya vifo hivyo vyote hutokea katika mataifa yanayoendelea. Je hali iko vipi kwa baadhi ya maatifa ya Afrika mashariki?

Kenya:

Kenya imekuwa ikishuhudia kiwango kikubwa cha vifo vya akina mama waja wazito. Kutokana na hilo serikali iliidhinisha sera ya utoaji huduma za bure kwa kina mama wanaojifungua katika taasisi za umma tagu Juni 2013.
Sera hii imekuwa ikiwawezesha wanawake waja wazito kupata huduma za bure wakati wa kujifungua katika vituo vya afya vya umma.
Mpango uliopo ni kwamba vituo hivyo vya afya hutoa huduma ya bure na baadaye serikali inavilipa kupitia wizara ya afya kulingana na idadi ya akina mama waliozalishwa.
Pia hakuna malipo yanayotolewa kwa huduma za kabla na baada ya kujifungua kwa akina mama na watoto kwa hadi wiki sita.
Licha ya huduma hiyo ya bure,kiwango cha hudumu zinazotolewa bado kinazusha maswali mengi huku baadhi ya wazazi katika hospitali hizo za umma wakiishia kujifungua katika hali duni na wengine hata kuishia kulala kitanda kimoja na wazazi wenzao.
Sio wengi wanaoweza kumudu gharama za hospitali za kibinafsi nchini.

Uganda:

Suala moja kubwa linalohusiana na afya ya uzazi ni nafasi ya akina mama kufikia huduma za dharura na za kiwango bora za uzazi na changamoto nyinginezo kwa wanawake nchini Uganda kufikia huduma hizi, zikiwemo gharama kubwa. Kama nchi nyingine nyingi zinazoendelea, Uganda inashuhudia kiwango kikubwa cha akina mama wanaofariki wakati wa kujifungua - jambo linalodhihirisha ufikiwaji wa huduma hizo za afya.
Hata wakati huduma hizo zinapatikana, kwa kawaida idadi ya wahudumu, dawa na vifaa hospitalini inakuwa ndogo ikilinganishwana idadi ya akina mama wanaohitaji hudumu hiyo.
Muongozo uliotolewa na shirika la Afya duniani ni kwamba mkunga mmoja anastahili kuwazalisha takriban wanawake 175 kwa mwaka, lakini wakunga nchini Uganda huwazalisha kati ya akina mama 350 hadi 500 kwa mwaka.
Upungufu na usambazaji mbovu wa wahudumu wa afya unaathiri kwa jumla gharama ya huduma ya afya ya uzazi na watoto.

Tanzania:

Idadi ya wanawake wanaofariki wakati wa uja uzito na kujifungua nchini Tanzania, kati ya 454 kwa kila visa 100,000 vya kujifungua - ni miongoni mwa zilizo kubwa duniani.
Licha ya kwamba serikali imeahidi kuisaidia hali, idadi hiyo ya vifo haijapungua

Post a Comment

0 Comments