humph the GREAT
Nianze kwa kumshukuru Mungu kwa kutupa afya njema mimi na wewe leo na kama kuna mtu anaumwa, basi kwa pamoja tumuombee apone haraka. Baada ya kusema hayo nizungumzie tozo za huduma ya kutuma au kupokea fedha kwa njia ya simu.
Nianze kwa kumshukuru Mungu kwa kutupa afya njema mimi na wewe leo na kama kuna mtu anaumwa, basi kwa pamoja tumuombee apone haraka. Baada ya kusema hayo nizungumzie tozo za huduma ya kutuma au kupokea fedha kwa njia ya simu.
Nasema hivyo kwa sababu tangu Julai Mosi
mwaka huu watu wamekuwa wakilalamika kwamba wanatozwa fedha nyingi kwa
kuwatumia fedha ndugu zao kwa njia ya simu.
Niliposikia malalamiko hayo nami nikajitosa kwa wakala mmoja ili nione kama walalamikaji wanasema kweli au ni porojo zao tu.
Nilikwenda kwa wakala mmoja nikiwa na
orodha ya ndugu zangu niliotaka niwatumie fedha kidogo kwa ajili ya
matumizi yao. Orodha hiyo ilikuwa na watu watano.
Nilipompa wakala wa kutuma fedha kwa
njia ya mtandao alisema kila fedha nitakayotuma pale sina budi kuongeza
shilingi 500 kama gharama ya kutuma fedha kwa ndugu zangu hao. “Ama
sivyo nikuingizie fedha hizo katika akaunti yako kisha utume mwenyewe,”
alinieleza wakala huyo wa mitandao ya kutuma fedha.
Nilifikiri kidogo nikaamua ni bora
nifanye hivyo ili nijue ni kiasi gani nitatumia kwa kuwatumia fedha watu
hao. Nilimpa fedha akaziingiza katika akaunti ya simu yangu.
Nilituma fedha kwa watu wale na
nikagundua kuwa kila niliyemtumia, nilikatwa shilingi 300, sikuwauliza
wapokeaji kama nao walitozwa fedha wakati wanachukua fedha
nilizowatumia.
Kwa watu wale watano niliowatumia fedha,
nilijikuta nikikatwa shilingi 1,500 jumla, si fedha ndogo ni nyingi
hivyo wahusika wanapaswa kuliangalia hili.
Nasema wanapaswa kuliangalia kwa sababu
ningeruhusu wakala anitumie kwa gharama alizonitajia ya shilingi 500 kwa
kila mtu, kwa watu watano, ningelipa shilingi 2,500.
Hiyo ni kwa mimi ambaye nipo jijini Dar
es Salaam, naamini huko mikoani wananchi watakamuliwa zaidi hasa kwa
kuwa baadhi yao hasa wale wa vijijini hawajui lolote, wanaweza kujikuta
wakitozwa gharama kubwa zaidi.
Niliwahi kumsikia mtu akisema ‘Ukitumiwa
shilingi 100,000 unakatwa shilingi 20,000.’ Nilimsogelea mtu yule na
kumwambia asipotoshe watu, si kweli hilo analolisema, yeye akajitetea
kuwa naye aliambiwa na mtu mwingine.
Mikanganyiko hiyo ndiyo iliyonifanya
nitumie muda wangu kutuma mwenyewe fedha lakini pia kuingia katika
utafiti mdogo kama mlivyoona hapo juu.
Ni jukumu sasa la vyombo husika kuchukua
muda wao kuelimisha jamii kuhusu makato anayokatwa mtumaji na mtumiwa
fedha ili kuepusha watu kuibiwa na mawakala wenye uroho wa kujitajirisha
haraka kwa kuwanyonya watu wasiojua.
Ni kawaida sana katika nchi yetu kungoja
kitu kilalamikiwe na watu na kelele zikiwa nyingi ndipo wahusika
hukuguta na kuanza kuelimisha umma kwa gharama kubwa, huku wananchi
wakiwa wameumia kama tulivyoona zoezi la kufungia simu feki, wakaguzi na
wadhibiti wa ubora wa simu hawakujali na sasa walalahoi ndiyo
wanaoadhibiwa kwa kuzimwa simu zao.
Ili watu wasiibiwe, haya mambo yawekwe hadharani mapema. Kinga ni bora kuliko tiba.
Jipu limepasuka, siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.
Tags
HABARI