Emanuel Lyabonga na Thomas Mhomba kukamatwa na meno ya tembo NJOMBE

humph the GREAT

                                Kamanda wa Polisi mkoani Njombe Pudensiana Protas

Jeshi la polisi mkoani Njombe linawashikilia vijana wawili wakazi wa mkoa jirani wa Iringa wakiwa na meno sita ya Tembo yenye uzito wa kilo 13.6 ambayo walikuwa katika harakati za kutafuta wateja.

Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Njombe Kamanda wa Polisi mkoani humo Pudensiana Protas amesema kuwa vijana hao wawili walikuwa na pikipiki ambapo polisi wakiwa doria katika kijiji cha Kitandililo wilaya ya kipolisi Makambako waliwakamata vijana hao baada ya kuwatilia shaka.

Kamanda Protas amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Emanuel Lyabonga na Thomas Mhomba wakazi wa Iringa na kwamba wamekamatwa na jeshi hilo wakiwa na pikipiki yenye namba za usajili MC 916 AWN.

Kuhusu thamani ya meno hayo Protas amesema kuwa wanasubiri wataalamu kutoka Idara ya maliasili ili kutambua thamani yake huku akitoa wito

Post a Comment

Please Select Embedded Mode To Show The Comment System.*

Previous Post Next Post