KENYA; balozi Dan kazungu kutoka Tanzania Kawa Waziri Kenya
habayloveHabay all info-
0
humph the GREAT
Kenyatta ateua mawaziri wapya Kenya, na balozi mpya Tanzania
Sambaza habari hii Facebook
Sambaza habari hi
Haki miliki ya pichaUHURU KENYATTA, FACEBOOK
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ametangaza watu anaopendekeza waidhinishwe kuwa mawaziri katika serikali yake mpya baada yake kushinda uchaguzi mwaka jana.
Mawaziri sita ambao walikuwa wanahudumu katika serikali yake muhula uliopita wamevuliwa uwaziri na kuteuliwa kuwa mabalozi.
Bw Dan Kazungu, ambaye amekuwa waziri wa madini, amependekezwa kuwa balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania.
Aliyekuwa balozi wa Kenya nchini humo Chirau Ali Mwakwere alijiuzulu mwaka jana ili kuwania kiti cha ugavana katika uchaguzi uliofanyika tarehe 8 Agosti.
Miongoni mwa walioteuliwa kuwa mawaziri wapya ni mwanahabari mkongwe Farida Karoney ambaye ameteuliwa kuwa waziri wa ardhi.
Wadhifa huo ulikuwa unashikiliwa na Prof Jacob Kaimenyi ambaye amependekezwa kuwa balozi wa Kenya katika Shirika la Umoja wa Mataifa kuhusu Sayansi, Elimu na Utamaduni (Unesco) mjini Geneva.
Bi Monica Juma ameteuliwa kuwa waziri mpya wa mambo ya nje kuchukua nafasi ya Amina Mohamed ambaye amependekezwa kuwa waziri wa elimu.
Mawaziri walioteuliwa kuwa mabalozi
Judi Wakhungu (Mazingira) - Ufaransa
Cleopa Mailu (Afya) - Umoja wa Mataifa mjini Geneva
Dan Kazungu (Madini) - Tanzania
Phylis Kandie (Leba na Jumuiya ya Afrika Mashariki) - Ubelgiji, Luxemburg na Umoja wa Ulaya
Willy Bett (Kilimo) - India
Jacob Kaimenyi (Ardhi) -UNESCO, Paris
Hassan Wario (Michezo) - Austria
Kwa sasa, orodha kamili ya mawaziri waliopendekezwa ni:
Adan Mohammed - Viwanda
Amina Mohammed - Elimu
Charles Keter - Kawi
Eugene Wamalwa - Ugatuzi
Farida Karoney - Ardhi
Fred Matiangi - Masuala ya Ndani na Usalama
Henry Rotich - Fedha (Hazina Kuu)
James Macharia - Uchukuzi
John Munyes - Madini na Mafuta
Joseph Mucheru - Teknolojia ya Habari na Mawasiliano