Theresa May ATANGAZA KUJIUDHURU UWAZIRI

humph the GREAT
 Theresa May 
Theresa May kujiuzulu kama kiongozi wa chama cha Conservative tarehe 7 Juni na kutoa fursa kuidhinishwa mchakato wa kuchaguliwa waziri mkuu mpya Uingereza.
Katika taarifa iliojaa hisia alioitoa huko Downing Street, Bi May amesema amefanya "kila awezalo" kutekeleza matokeo ya kura ya maoni kuhusu EU ya mnamo 2016.
Ni jambo linalosalia kuwa "na majuto mengi" kwamba ameshindwa kutimiza Brexit - Uingereza kujitoa katika Umoja wa Ulaya, ameongeza.
Lakini waziri mkuu mpya ndio suluhu " kwa manufaa ya taifa"



Mpango wa Theresa May wa Uingereza kujiondoa katika Umoja wa Ulaya umepingwa na wabunge kwa mara ya pili huku zikiwa zimesalia siku 17 hadi muda wa taifa hilo kujitoa katika EU.
Wabunge walipiga kura kupinga mpango wa waziri mkuu huyo kwa kura 149 - kiwango kidogo ikilinganishwa na kura zilizopigwa Januari.
Bi May amesema wabunge sasa watapiga kura iwapo Uingereza iondoke katika EU bila ya mpango na iwapo hatua hiyo itashindwa, kura ya iwapo mpango mzima wa kujiondoa - Brexit uahirishwe.
Waziri mkuu aliwasilisha ombi la dakika ya mwisho kwa wabunge waunge mkono mpango wake baada ya kupata hakikisho kisheria kuhusu msimamo wa Ireland kuhusu kujitoa katika EU.

Mpango wa Bi May ni upi?

Akifafanua mpango wake, amesema wabunge watarudi tena kupiga kura Jumatano kuhusu iwapo Uingereza inastahili kuondoka EU na mpango au bila mpango.
Iwapo watapiga kura kupinga mpango , watapiga tena kura siku inayofuata kuhusu iwapo kuidhinisha kurefushwa kwa kipengee cha Article 50 - mfumo wa sheria utakao iondoa Uingereza katika EU kufikia Machi 29.

Bi May amesema wabunge itabidi waamue iwapo wanataka kuahirisha Brexit, kuandaa kura nyingine ya maoni au iwapo "wanataka kuondoka na mpango lakini sio mpango ulioko".

Bi May amesema ataendelea kuhudumu kama waziri mkuu wakati kukitarajiwa kuidhinishwa mchakato wa kumchagua kiongozi mpya wa chama cha Conservative.
Atajiuzulu kama kiongozi wa chama hicho Juni 7 na uteuzi wa waziri mkuu mpya unatarajiwa kuanza wiki inayoafuata baada ya hatua hiyo.


Post a Comment

Please Select Embedded Mode To Show The Comment System.*

Previous Post Next Post