Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Ticker

6/recent/ticker-posts

HAKIKISHA HUBANDUKI NJIA KUU- 5


KUNA manufaa makubwa ya kuheshimu ndoa/penzi lako. Kikubwa ni utulivu wa akili yako mwenyewe. Tambua kwamba unapochepuka, unakuwa unajiingizia mzigo kichwani ambao hauna sabababu yoyote. Utakuwa mtu wa wasiwasi wa kujitakia.
Ukipigiwa simu mbele ya mwezi wako unaanza kuchachawa. Ukisasahau simu nyumbani akili inaruka kwa kuchanganyikiwa. Badala ya kulala unakuwa kama mlinzi, unamvizia mwenzio alale asije kushika simu yako. Akiamka kwenda kujisaidia na wewe unakurupuka kisha unamfuatilia hatua zote mpaka atakaporejea kitandani, unahofia atashika simu na kukukagua!
Wasiwasi wa nini? Baki njia kuu! Tuendelee na kisa cha Mama Dennis aliposaliti ndoa kwa dereva taksi, wiki iliyopita aliishia hapa: “Nilijisikia vibaya sana lakini sikutaka kuzungumza. Kwa kawaida mume wangu huwa hakamilishi ngwe bila kushauriana.
“Nikimwambia bado, basi ataendelea kuzungusha mashine yake kwa umaridadi wa hali ya juu mpaka aone nimefanikiwa kupanda kileleni ndipo naye hunishusha kwa utulivu ambao binafsi huufurahia.
“Nakumbuka ni utaalamu huo wa mume wangu ndiyo ulionifanya nipagawe kwake nikiwa binti mdogo kabisa. Nikaapa huyo ndiye atakuwa mwanaume wangu wa ndoa.
Kweli, nilifanya juu chini, nikatumia kila njia kuhakikisha namfanya anione mimi ndiye mwanamke sahihi wa kuoa, na kweli nilifanikiwa.
“Nashangaa pamoja na kulitambua hilo lakini nikadata kwa Sos, dereva taksi mjanjamjanja ambaye kwa kumlinganisha, thamani yake hailingani hata na ukucha wa mume wangu ambaye ni mwanaume mwenye heshima zake na naamini wanawake wengi wanammezea mate.
“Hayo huwa najilaumu lakini haisaidii kwa sababu ni maumivu baada ya matokeo, yaani ni majuto baada ya aibu ambayo niliipata. Nikirudi pale kitandani, baada ya Sos kukamilisha mzunguko wa kwanza, akiniacha njiani bila kunifikisha, alitoka nje kisha akarudi ameshikilia soda mbili baridi.
“Akanifungulia moja nikainywa, kweli nilikuwa na kiu.
Alitoka tena na kurejea baada ya muda mfupi mkononi akiwa na sahani mbili za chipsi kwa kuku. Nilijiuliza zimetengenezwa wapi, ikabidi nimuulize. Akaniambia alizinunua kabisa kabla hajanipitia kazini na pale nyumbani alifanya kuzipasha moto kwa kutumia ‘microwave’.
“Nilizipokea zile chipsi na kuanza kuzila kwa harakaharaka, maana njaa ilikuwa kali sana. Tulipomaliza kula Sos alitaka kunivamia tena, hapo ilibidi nimzuie, nilimwambia ni lazima asubiri chakula kiteremke vizuri ndipo mambo mazuri yanaweza kufanyika sawasawa.
“Sos alinielewa kwa shingo upande. Tulisubiri kwa dakika chache Sos uvumilivu ulimshinda, akanivamia tena, hapo nikawa sina kipingamizi. Awamu hii bora hata ile ya kwanza, maana alipojiridhisha tu kuwa barabara inapitika, yeye aliwasha gari na kuanza kuendesha kwa kasi.
“Hakutaka kujadiliana na mimi dereva mwenzake kwa chochote, matokeo yake akafika mwisho wa safari wakati mimi ndiyo nilikuwa naanza kuchanganya. Niliumia sana tena sana! Wakati najilaumu, Sos akaniambia twende tukaoge ili tuwahi kuondoka kwa sababu huo ni muda wa mwenye nyumba kurejea nyumbani.
“Ni hapo ndipo nikathibitisha ukweli kwamba pale siyo kwake isipokuwa alinipeleka kwa watu. Nilijisikia vibaya sana. Mimi ni mwanamke na heshima zangu, mume wangu ni mtu wa maana sana, ni kiongozi sehemu yake ya kazi, akiwa kwenye kiti chake ofisini, watu wanamnyenyekea sana.
“Eti pamoja na hayo yote, nikajisahau na kuangukia kwa dereva taksi ambaye hana mbele wala nyuma. Kitandani hajiwezi, ukiachana na hilo, anaonekana ni mhuni asiyejiheshimu. Mtu mwenye heshima zake hawezi kunichukua mimi mke wa mtu na kwenda kulala naye kwenye nyumba ya rafiki yake.
“Kuna mambo mawili nikawa nimejiongeza. La kwanza ni kuwa Sos hana siri kwa sababu mpaka apewe ufunguo wa nyumba na rafiki yake lazima atakuwa amemueleza matumizi yake, kwa hiyo bila shaka alimweleza waziwazi kuwa anakwenda kulala na mimi. Nilipowaza hivyo nilijihisi kuvuliwa nguo, maana hakuna siri tena.
“Ina maana kuwa huyo rafiki yake atawaambia wenzake ambao kwa hakika watakuwa wananijua. Nilijua huyo rafiki wa Sos atakuwa dereva taksi mwenzake. Jambo la pili ambalo nilijiongeza ni kuwa kabla ya Sos kunifuata, atakuwa aliwaambia wenzake. Natambua kuna wanaume wana tabia ya kuchanganyikiwa kwa wanawake kisha kuwafanya matangazo.
“Nilivyomuona Sos, nilimfananisha na mwanaume wa aina hiyo lakini haikuwa na maana kubwa sana kwa sababu tayari nilishamfungulia mlango, akaingia, mwili wangu akautumia. Nikiwa bado nimekaa pale kitandani, niliwaza sura yangu nitaiweka wapi mbele ya wale madereva taksi.

Post a Comment

0 Comments