BASI LAUA ZAIDI YA ABIRIA 40 BAADA YA KUANGUKIWA NA KONTENA IRINGA

humphrey the GREAT














ABIRIA zaidi ya 40 wanahofiwa kufariki dunia baada ya basi la Majinja Express ambalo lilikuwa likitokea Mbeya kwenda Dar es Salaam kufunikwa na kontena maeneo ya Changalawe, Mafinga mkoani Iringa muda huu.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo ni kwamba dereva wa basi alikuwa akijaribu kulipita lori ndipo walipodondokewa na kontena hilo.
Inadaiwa kuwa basi hilo lilikuwa limebeba abiria 65 na abiria nane tu ndiyo walionusurika katika ajali hiyo mbaya.

WALAZWE PEMA PEPONI NA POLENI SANA NDUGU, RAFIKI NA FAMILIA WA MAREHEMU.

Post a Comment

Please Select Embedded Mode To Show The Comment System.*

Previous Post Next Post