humph the GREAT
Akizungumza
na gazeti hili, mama mzazi wa marehemu na mtuhumiwa, aliyejitambulisha
kwa jina la Mwaija Bakari (pichani) alisema awali, Majaliwa alikuwa
mlevi wa kupindukia, lakini hivi karibuni alikwenda kwa kiongozi mmoja
wa dini, akiomba maelekezo ya namna ya kuacha pombe.
Mama mzazi wa marehemu na mtuhumiwa, Mwaija Bakari.
Humphrey, blogger
MAJALIWA Mzaramingo, mkazi wa
Chalinze mkoani Pwani, amemuua kaka yake kwa kumpiga kichwani na mchi,
ikidaiwa ni laana iliyotokana na kushindwa kutekeleza masharti
aliyopewa, baada ya kunyonya titi la mama yake mzazi.
“Ukweli tukio hili linanipa uchungu
sana, kwani sasa ni kama nimeshapoteza watoto wawili kwa mpigo, ukweli
mtuhumiwa alikuwa na tabia ya ulevi uliopindukia na hivi karibuni
alikwenda kwa ustaadhi f’lani akamuelekeza jinsi ya kuacha pombe.
“Ustaadhi huyo alimwambia aje aniambie
nilioshe ziwa langu la kushoto, kisha alinyonye huku akinuizia na maji
niliyooshea mengine ampelekee.
“Mwanangu alifanya hivyo na mwanzoni
aliacha kabisa pombe, lakini siku za hivi karibuni alirudia tena kwa
kasi, ingawa ustaadhi huyo alishamuonya kuwa kama angerudia kuonja
kilevi basi yatakayomtokea asije kumfuata tena.
“Sasa siku ya tukio wote tukiwa hapa
nyumbani marehemu Mwalimu alikuwa akijisikia homa hivyo hakwenda kazini.
Mtuhumiwa alimwambia kaka yake wachange ili wanunue kitoweo kwa ajili
ya chakula cha jioni.
“Marehemu alimwambia mdogo wake kuwa leo sina pesa, si unajua mimi naumwa sijatoka kwenda kutafuta.
“Baada ya kusikia hivyo mtuhumiwa alianza kumshutumu kaka yake kuwa alikuwa na pesa lakini alijifanya bahili ili amtegee.
“Hivyo Majaliwa alienda kununua nyama na
kumpa mkewe apike, lakini akaagiza kaka yake asipewe hata kipande
kimoja kwa kuwa hakuchangia chochote.
“Mkewe alikarangiza na ulipofika muda wa kula, kwa kuwa mtuhumiwa hakuwepo, mkewe akamchotea kidogo shemeji yake.
“Wakati marehemu akiendelea kutafuna,
mtuhumiwa alitokea ghafla na kumuuliza kwa nini alikuwa akila kitoweo
ambacho alimuagiza asikiguse.
“Hali hiyo ilizua malumbano kabla ya
Majaliwa kuchukua mchi wa kutwangia na kumpiga nao kaka yake kichwani
mara tatu, alianguka na kuanza kugaragara.“Nilipoona hali hiyo nilianza
kupiga mayowe kuomba msaada, wasamaria wema walifika lakini mtuhumiwa
alishakimbia. Tulimkimbiza zahanati ya serikali hapa jirani lakini
walisema hali yake ilikuwa mbaya hivyo tumkimbize Hospitali ya Rufaa ya
Tumbi iliyopo Kibaha.
“Tukiwa maeneo ya Kongowe kuelekea Tumbi
mwanangu aliaga dunia, jamani sasa nimekosa watoto wawili kwa mpigo,
huyu amekufa na mtuhumiwa naye siwezi kuwa naye tena ni lazima atafia
jela,” alisema mama huyo huku akilia.
Kufuatia tukio hilo, waandishi wetu
walimpigia simu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, ACP Bonaventura Mshongi
lakini simu yake haikuwa hewani.
Marehemu alizikwa kijijini hapo Juni 30, mwaka huu.
Tags
HABARI